Wednesday, 8 July 2015
10:30
Unknown
No comments
CHAMA Cha Mapinduzi (CCM) kimesema hakitachagua mgombea wa kiti cha urais kwa presha za wapambe wa wagombea.
Chama hicho ambacho kimeanza vikao vyake kabla ya kupata mgombea wa nafasi hiyo katika uchaguzi mkuu, kimesema hakitarajii kuona walioomba kuteuliwa wakihamia upinzani baada ya majina yao kukatwa, kwani kanuni za chama zinajulikana.
Alisema watangaza nia wanafahamu kwamba upo mchujo, ambao kwa kuanzia, watapatikana watu watano, baadaye watatu na kisha mgombea mmoja atakayepitishwa.
Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Nape Nnauye alisema hayo mjini hapa jana katika mkutano wake na waandishi wa habari.
“CCM haitafanya uamuzi kutokana na msukumo wa wapambe wa wagombea, kwani kuna kanuni na taratibu na waliochukua fomu wanafahamu kuna kushinda na kushindwa, na asiyekubali kushinda hatakuwa mshindani,” alisema.
Alisema presha za wapambe wa mitaani haziwezi kukipa chama taabu, kwani kina utaratibu wake na jambo la muhimu ni kuhakikisha hatua zote zinafuatwa. “Sioni mtu atakayeondoka kwenye chama mara baada ya jina lake kukatwa, ni maneno tu, na wapambe pia ni sehemu ya presha, kwa nini aondoke,” alisema.
CHANZO HABARI LEO
Subscribe to:
Post Comments (Atom)


0 comments:
Post a Comment