Monday, 6 July 2015

WABUNGE jana walipitisha Muswada wa Sheria ya Petroli wa Mwaka 2015, ambao ni miongoni mwa miswaada ya sekta ya mafuta na gesi iliyokuwa ikipigiwa kelele na wabunge wa upinzani.
Miswada mingine iliyokuwa ikipigiwa kelele, ambayo pamoja na huo wa petroli iliwasilishwa kwa pamoja bungeni juzi ni Muswada wa Sheria ya Usimamizi wa Mapato ya Mafuta na Gesi wa Mwaka 2015 na Muswada wa Sheria ya Uwazi na Uwajibikaji katika Tasnia ya Uchimbaji Tanzania wa Mwaka 2015.
Kutokana na hali hiyo wabunge zaidi ya 40 wa kambi ya upinzani kutoka vyama vinavyounda Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa), walitolewa nje ya Bunge Ijumaa na juzi kutokana na kufanya fujo wakati wa hatua za kutaka kusomwa kwa miswada hiyo.
Baadhi ya wabunge hao wamefungiwa kuhudhuria vikao vyote vilivyobaki vya Bunge hilo na baadhi wamesimamishwa kuhudhuria vikao viwili na wengine vitano mfululizo.
Spika wa Bunge, Anna Makinda alisema muswada huo ulipitishwa kwa kauli moja kwa wabunge kuitikia kwa kusema ndiyo, wakati waliosema hapana hawakuwepo, hivyo sasa unasubiri Rais Jakaya Kikwete ausaini ili uwe sheria.
Mbunge wa upinzani aliyekuwepo ni Hamad Rashid Mohammed (CUF-Wawi). Miswada hiyo iliingia kwikwi kuwasilishwa bungeni baada ya semina ya wabunge Jumanne iliyopita iliyoandaliwa na Wizara ya Nishati na Madini mjini hapa, ambapo wabunge wengi waliochangia siku hiyo waliomba serikali isifanye haraka kuiwasilisha kwani muda hautoshi kujadili masuala hayo nyeti.
Akichangia muswada wa mafuta kwa kujibu baadhi ya hoja za wabunge jana, Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Charles Mwijage, alisema baadhi ya watu wanapinga muswada huo kwa sababu unatoa nafasi ya asilimia 25 kwa kampuni ya Taifa, pia umeunda mamlaka ya udhibiti na pia hawapendi ushiriki wa serikali katika masuala ya mafuta na ges.
CHANZO HABARI LE0

0 comments:

Post a Comment

wanaotutazama


hit counter

tz shiling exchange

MY CALENDAR

Total Pageviews

Recent Posts

find us on twitter

Find Us On Facebook

MATANGAZO