Wednesday, 8 July 2015

Wiki hii maskio yote ya Watanzania yanaelekezwa mjini Dodoma, mji mkuu wa Tanzania ambapo chama tawala nchini humo Chama Cha Mapinduzi (CCM) kinamchagua mtu mmoja atakayepeperusha bendera ya chama hicho katika uchaguzi mkuu wa wabunge na rais unaotarajiwa kufanyika tarehe 25 Oktoba 2015.
Vikao vya mchakato huo vinaanza rasmi Jumatano huku vikitanguliwa na kikao cha Kamati ya Ulinzi na Usalama ambayo kimsingi pamoja na mambo mengine kitapitia wasifu wa watia nia wote lakini pasipo kupunguza jina lolote.
Siku ya Alhamisi (09 Julai), Kamati Kuu ya chama yenye wanachama takribani 32 itakutana na hapo ndipo upungazaji wa majina utafanyika hadi kufikia majina matano tu.
Baada ya hapo, Halmashauri kuu ya chama itakutana siku ya Ijumaa tarehe 10 Julai ambapo itachuja majina hayo matano hadi kufikia matatu kupitia mtindo wa kupiga kura. Majina haya matatu ndiyo yatakayokwenda katika Mkutano Mkuu wa Chama ambao ndio utakaochagua jina moja la huyo mgombea urais kwa tiketi ya chama
Mkutano Mkuu huu unajumisha takribani wanachama 2100 ikiwa ni pamoja na Wabunge wa CCM Tanzania bara na wawakilishi wengine kutoka Zanzibar lakini pia wawakilishi wa chama kutoka ngazi mbalimbali hadi zile za chini.
CHANZO BBC

0 comments:

Post a Comment

wanaotutazama


hit counter

tz shiling exchange

MY CALENDAR

Total Pageviews

Recent Posts

find us on twitter

Find Us On Facebook

MATANGAZO