Papa Francis amewasili Kenya katika ziara yake ya kwanza ya kihistoria
barani Afrika bara linalokabiliwa na changamoto za kiusalama. Mamilioni
wanatarajiwa kuhudhuria misa Nairobi.
Papa huyo mwenye umri wa miaka 78 ni wa tatu kuzuru bara hilo,pia
amepangiwa kutembelea Uganda na Jamhuri ya Afrika ya kati inayokumbwa na
vita kwa ziara ya siku sita.
Katika mitaa ya jiji kuu la Kenya Nairobi ambako kiongozi huyo wa kanisa
katoliki ulimwenguni anatarajiwa kuwasili mwendo wa saa kumi na moja
jioni, huku mabango makubwa yametundikwa kumkaribisha.
Umati wa watu unatarajiwa kujitokeza kulaki msafara wake.Gazeti la the
Standard nchini Kenya liliandika kichwa "Karibu Papa Francis"
kumkaribisha huku ujumbe huo ukirudiwa kwa lugha ya kilatini Grata
Franciscus Pontifex.
Papa Francis atalakiwa nchini Kenya na Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta.
Katika Ikulu ya Nairobi atakako kuwa na mazungumzo na Rais Uhuru
Kenyatta, Papa Francis anatarajiwa kugusia swala la Ufisadi na tofauti
iliyopo kati ya masikini na tajiri, maswala ambayo ni muhimu kwa
wakenya.
Kiongozi huyo ataongoza misa itakayohudhuriwa watu karibu 500,000 siku
ya Alhamisi. Nchini Uganda miongoni mwa mengine atazuru mahala
walikozikwa viongozi wa kikristo waliouliwa nchini humo. Papa Francis
anatarajiwa kutumia gari rasmi lililo wazi ambalo hulitumia anapofanya
ziara .
Wednesday, 25 November 2015
Subscribe to:
Post Comments (Atom)


0 comments:
Post a Comment