Wednesday, 25 November 2015

Papa Francis amewasili Kenya katika ziara yake ya kwanza ya kihistoria barani Afrika bara linalokabiliwa na changamoto za kiusalama. Mamilioni wanatarajiwa kuhudhuria misa Nairobi.
Papa huyo mwenye umri wa miaka 78 ni wa tatu kuzuru bara hilo,pia amepangiwa kutembelea Uganda na Jamhuri ya Afrika ya kati inayokumbwa na vita kwa ziara ya siku sita.
Katika mitaa ya jiji kuu la Kenya Nairobi ambako kiongozi huyo wa kanisa katoliki ulimwenguni anatarajiwa kuwasili mwendo wa saa kumi na moja jioni, huku mabango makubwa yametundikwa kumkaribisha.
Umati wa watu unatarajiwa kujitokeza kulaki msafara wake.Gazeti la the Standard nchini Kenya liliandika kichwa "Karibu Papa Francis" kumkaribisha huku ujumbe huo ukirudiwa kwa lugha ya kilatini Grata Franciscus Pontifex.
Papa Francis atalakiwa nchini Kenya na Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta. Katika Ikulu ya Nairobi atakako kuwa na mazungumzo na Rais Uhuru Kenyatta, Papa Francis anatarajiwa kugusia swala la Ufisadi na tofauti iliyopo kati ya masikini na tajiri, maswala ambayo ni muhimu kwa wakenya.
Kiongozi huyo ataongoza misa itakayohudhuriwa watu karibu 500,000 siku ya Alhamisi. Nchini Uganda miongoni mwa mengine atazuru mahala walikozikwa viongozi wa kikristo waliouliwa nchini humo. Papa Francis anatarajiwa kutumia gari rasmi lililo wazi ambalo hulitumia anapofanya ziara .

0 comments:

Post a Comment

wanaotutazama


hit counter

tz shiling exchange

MY CALENDAR

Total Pageviews

Recent Posts

find us on twitter

Find Us On Facebook

MATANGAZO