Friday, 6 November 2015
01:14
Unknown
No comments
RAIS mstaafu wa Serikali ya Awamu ya Nne, Jakaya Kikwete ametoa msamaha kwa wafungwa 4,160 katika kuaga na kukabidhi madaraka ya Serikali kwa Rais wa Awamu ya Tano, Dk John Magufuli.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mathias Chikawe kwa vyombo vya habari Dar es Salaam, kati ya wafungwa hao,wafungwa 867 wataachiwa huru na wafungwa 3,293 watapunguziwa vifungo vyao na kubaki gerezani wakitumikia sehemu ya vifungo vyao vilivyobaki.
Kwa mujibu wa Chikawe,msamaha hautawahusu wafungwa wenye adhabu za kunyongwa,waliohukumiwa kunyongwa na adhabu hiyo baadaye kubadilishwa kuwa kifungo cha maisha au kifungo gerezani.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)


0 comments:
Post a Comment