Uongozi wa shirika la umeme nchini Tanesco umewafukuza kazi wafanyakazi saba waandamizi wa shirika hilo wakiwemo mameneja kutokana na makosa mbalimbali ikiwemo vitendo vya wizi, kudai rushwa, ubadhirifu wa mali wa shirika hilo pamoja na kutoa lugha chafu kwa wananchi jambo ambalo ni kinyume na taratibu za maadili ya kazi na uongozi huo kuwaonya wafanyakazi wengine wenye tabia kama hizo kwamba watachukuliwa hatua.
Mkurugenzi mkuu wa shirika hilo Mhandisi Felichesm Mramba akitoa
taarifa juu ya uumuzi wa kufukuzwa kazi kwa wafanyakazi hao saba kwa
waandishi wa habari jijini Dar es Salaam amesema uamuzi huo umechukuliwa
ikiwa ni mpango endelevu wa shirika la Tanesco kuimrisha nidhamu kwa
wafanyakazi wake kutambua wajibu wao wa kutoa huduma ya nishati kwa
wananchi na sio na sio kuwasumbua wateja na kutaja vitengo ambavyo
wafanyakazi hao wamefukuzwa ikiwemo ngazi ya mameneja, wahandisi na
wahasibu kutoka mikoa ya Kinondini kaskazini, Katavi, Kagera na Ilala.


0 comments:
Post a Comment