Tuesday, 17 November 2015


Job Ole Ndugai ndie spika mpya wa bunge la Tanzania. Ndugai mwenye umri wa miaka 55 alijipatia thuluthi mbili ya kura zinazohitajika.
Alikuwa naibu wa spika wa bunge lililokamilika.
Ndugai anatarajiwa kuliongoza bunge lenye zaidi ya wabunge 100 kutoka upinzani ,ikiwa ndio idadi kubwa zaidi kuwahi kuchaguliwa katika bunge hilo.
Kulikuwa na wagombea 8 waliowania wadhfa huo wa spika,lakini mwishowe ushindani ulikuwa kati ya mgombea wa chama tawala cha CCM Job Ole Ndugai na mwenzake wa upinzani Goodluck Ole Medeye kutoka chama cha Chadema.
Bunge jipya litakuwa na wanachama 394,ikiwa linawawakalishi 30 zaidi ikilinganishwa na bunge lililopita kufuatia kubuniwa kwa maeneo mapya ya ubunge.

0 comments:

Post a Comment

wanaotutazama


hit counter

tz shiling exchange

MY CALENDAR

Total Pageviews

Recent Posts

find us on twitter

Find Us On Facebook

MATANGAZO