Friday, 2 October 2015

Ndege za kijeshi za Jeshi la Wananchi wa Tanzania, JWTZ.
MARUBANI wawili wa Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ), wanahofiwa kufa maji baada ya ndege yao ya mazoezi, kuangukia katika mwambao wa Bahari ya Hindi eneo la Visiwa vya Mbudya, Kaskazini Mashariki mwa Jiji la Dar es Salaam.
Kwa mujibu wa taarifa ya Kurugenzi ya Habari na Mahusiano ya JWTZ Makao Makuu, ajali hiyo ilitokea jana majira ya saa 3.30 asubuhi. Ilisema mara baada ya ajali hiyo, marubani wake, Luteni Kanali Talkisiyo Bruno Ndongoro na Kapteni Gaudence Peter Hamis walipotea.
Taarifa hiyo iliongeza kuwa, chanzo cha ajali hiyo ni hitilafu ya injini, jambo ambalo limeelezwa marubani hao walipoligundua, walifanya juhudi za kujiokoa kutoka katika ndege hiyo, kwa bahati mbaya waliangukia baharini na kuzama. Kutokana na tukio hilo, JWTZ imetoa taarifa ikisema inaendelea kuwatafuta marubani hao kwa kutumia boti za kijeshi. chanzo habari leo


0 comments:

Post a Comment

wanaotutazama


hit counter

tz shiling exchange

MY CALENDAR

Total Pageviews

Recent Posts

find us on twitter

Find Us On Facebook

MATANGAZO