Joto limepanda mjini hapa, ambapo mchujo wa kumpata mgombea urais wa
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM),
unaanza rasmi leo, pale Kamati Kuu (CC) itakapochuja majina ya watangaza
nia 38 waliochukua na kurejesha fomu na kubakiza watano.
Kamati Kuu itachuja majina ya watangaza nia hao huku ikizingatia kile
kilichochambuliwa na kupendekezwa na Kamati ya Ushauri ya CCM,
inayoundwa na wazee wastaafu, iliyokutana hivi karibuni na pia Kamati ya
Nidhamu na Usalama, iliyokutana kwa siku nzima jana chini ya Mwenyekiti
wa CCM Taifa, Rais Jakaya Kikwete.
Kamati ya Maadili na Usalama iliyokutana jana, ilihusisha wajumbe
kutoka CCM na serikalini wakiwemo watendaji wa Taasisi ya Kuzuia na
Kupambana na Rushwa (Takukuru) na Idara ya Usalama wa Taifa.CHANZO HABARI LEO
Friday, 10 July 2015
Subscribe to:
Post Comments (Atom)


0 comments:
Post a Comment